Posts

KLINIKI YA MSAADA WA KISHERIA MOROGORO: WANANCHI WAPATIWA HUDUMA ZA HAKI KARIBU NA MAKAZI YAO.

Image
                                                    Katika Stendi ya Zamani ya Mabasi, Manispaa ya Morogoro Mjini, wananchi wanaendelea kunufaika na huduma za msaada wa kisheria zinazotolewa kupitia banda la Wizara ya Katiba na Sheria. Kupitia Kliniki ya Msaada wa Kisheria, mwananchi amekabidhiwa hati ya kiapo kwa ajili ya kuwasilishwa mahakamani ili kumuwezesha kuwa msimamizi wa mirathi. Huduma hii ni sehemu ya jitihada za serikali kusogeza haki karibu na wananchi, kutoa elimu ya kisheria, na kusaidia jamii kutatua changamoto zao za kisheria kwa urahisi na ufanisi.  

Wananchi Wamiminika Morogoro Kupata Huduma za Msaada wa Kisheria Bila Malipo

Image
Mamia ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro wamejitokeza kwa wingi katika Kliniki Maalumu ya Msaada wa Kisheria inayofanyika katika viwanja vya Standi ya Zamani, Manispaa ya Morogoro. Kliniki hiyo imeandaliwa na Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Dawati la Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na Dawati la Jinsia la Jeshi la Polisi, Wakala wa Usajili, Ufilisi na Usaili (RITA) pamoja na Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS). Huduma zinazotolewa katika kliniki hiyo ni pamoja na ushauri wa kisheria, elimu ya haki za binadamu, masuala ya mirathi, ndoa na talaka, usajili wa vizazi na vifo, masuala ya ukatili wa kijinsia, pamoja na migogoro ya ardhi na ajira. Kliniki hiyo inafanyika kwa muda wa siku mbili mfululizo, ikiwa na lengo la kuwafikia wananchi wengi zaidi hususan wale wasiokuwa na uwezo wa kugharamia huduma za kisheria. Kwa manufaa ya umma wa Tanzania, kliniki kama hizi zinachangia kuimarisha utawala wa sheria, kupunguza migogoro isiyo ya lazima, na kujenga jamii yenye uelewa wa haki, usaw...

Waziri Juma Homera Akagua Utendaji wa Taasisi za Katiba na Sheria Morogoro

Image
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Juma Homera, amefanya kikao maalum na watendaji walio chini ya Wizara hiyo katika Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kuakisi na kutathmini utendaji wa Wizara na taasisi zake katika mkoa huo. Kikao hicho kimewakutanisha viongozi na watumishi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali (OSG), Mahakama ya Tanzania pamoja na Wakala wa Ufilisi na Usaili (RITA). Katika mkutano huo, Mhe. Homera alisikiliza taarifa za utekelezaji wa majukumu, changamoto zinazowakabili watendaji pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika utoaji wa huduma za haki na kisheria kwa wananchi wa Mkoa wa Morogoro. Waziri alisisitiza umuhimu wa uwajibikaji, ushirikiano wa taasisi na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kuboresha utoaji wa huduma na kuimarisha haki, usawa na utawala wa sheria. Mhe. Homera aliwahimiza watendaji hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi, akibainisha kuwa Wizara itaendelea kutoa ushirikiano na maboresho yatakayowezesh...

JE NI AINA ZIPI ZA NDOA ZINAZOTAMBULIWA KISHERIA NCHINI TANZANIA ..?

Image
 

KWANINI UHAKIKI WA UMILIKI NI MUHIMU KABLA YA KUFANYA MALIPO YA ARDHI.. ?

Image
 

JE .! UNAZIJUA NYARAKA ZINAZOHITAJIKA KATIKA MAUZO YA ARDHI..?

Image
 

JE UNAIJUA HAKI YA MTOTO, IJUE SASA.... !

Image