Posts

Showing posts from January, 2025

KILIMANJARO WANANCHI WAJITOKEZA KWA WINGI KUPATA ELIMU NA MSAADA WA KISHERIA: MATUKIO KATIKA PICHA

Image
Mnamo tarehe 29 Januari 2025, Wizara ya Katiba na Sheria ilizindua Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Mkoa wa Kilimanjaro. Uzinduzi huo ulifanyika katika viwanja vya Stendi ya zamani, ambapo wananchi walijitokeza kwa wingi kupata huduma za kisheria.  Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, aliongoza uzinduzi huo na kueleza kuwa kampeni hii inalenga kutatua migogoro mbalimbali inayowakabili wananchi.  Alisisitiza kuwa kampeni hii ni utekelezaji wa dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha wananchi wanapata haki zao kwa urahisi.  Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, aliwahimiza wananchi kutumia fursa hii kupata elimu na msaada wa kisheria ili kutatua changamoto zinazowakabili. 
Image
 KUANDIKA WOSIA SIO KUJICHULIA KIFO-MSLAC Elimu ya usimamizi wa mirathi imeendelea kutolewa na timu ya wataalamu wa Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia ambapo wananchi wametakiwa kuzidi kuwa na tabia ya kuandika wosia ili kuondoa sintofahamu kwa ndugu wanaobaki pindi wanapofariki. Akizungumza mratibu wa mradi huo Halmshauri ya Tanganyika Pendoveera Nyanza amewataka wakazi wa Kata za Karema na Kapalamsenga zilizopo katika mwambao za Ziwa Tanganyika mkoa mkoani Katavi, kuondoa dhana potofu ya kuwa endapo ataandika wosia mapema ni kujichulia kifo.  Kwa upande wake Christina Ngalikiliwi kutoka dawati la Jinsia na watoto halmashauri ya Tanganyika amewataka wanandoa kuacha kufanyiana ukatili kwani matendo hayo hupelekea familia kusambaratika hali inayozalisha watoto wa mtaani. Aidha amekemea matendo ya ubakaji na ulawiti yanayofanywa na watu wazima dhidi ya watoto kwani hukatisha ndoto za watoto na kuwakosesha haki zao za msingi. Mussa Kassim mkazi wa Karema amekiri uwepo wa...
Image
  UZINDUZI WA MSLAC MKOANI KILIMANJARO, KATIKA PICHA

Image
Mafunzo Yawapa Nguvu Wataalamu Halmashauri Kilimanjaro: Mkakati wa Mama Samia Legal Aid Campaign Wapewa Msukumo Mpya Mafunzo haya yaliwalenga wataalamu wa ngazi ya halmashauri mkoani Kilimanjaro ili kuwajengea uwezo katika kuendesha, kusimamia, na kutathmini Mpango wa Mama Samia Legal Aid Campaign. Lengo kuu ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata msaada wa kisheria kwa wepesi, uwazi, na ufanisi. Uelewa wa Mkakati wa Mama Samia Legal Aid Campaign: Mkakati wa Msingi:   Unajumuisha kutoa elimu ya kisheria kwa wananchi, kuimarisha upatikanaji wa haki, na kuboresha mifumo ya usimamizi wa rasilimali za kisheria. Umuhimu kwa Maendeleo ya Jamii:   Kupitia mpango huu, wananchi wanakuwa na uelewa mpana wa haki zao, hivyo kukuza amani, ushirikishwaji na maendeleo endelevu katika jamii. Mwongozo wa Uendeshaji na Mambo ya Kuzingatia: Usimamizi Madhubuti:   Wawezeshaji wanapaswa kuandaa ratiba inayozingatia mahitaji ya kila eneo na kufuata taratibu za utawala bora. Ushirikiano Miongoni ...