
SERIKALI YAWANOA MABALOZI NA WAJUMBE 8000 SONGEA: MIKAKATI YA KIKATIBA YA KUIMARISHA UTATUZI WA MIGOGORO KWA AMANI,DEMOKRASIA NA MASWALA YA UCHAGUZI MKUU UJAO Mpango wa kutoa elimu ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala kwa mabalozi na wajumbe wa serikali za mitaa unalenga kuimarisha misingi ya utawala bora, haki za binadamu, na amani ya kijamii kama inavyobainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (kama ilivyorekebishwa). 1. Msingi wa Kikatiba wa Mpango huu Mpango huu unajikita katika matakwa ya Ibara ya 8(1)(a)(b) ya Katiba, ambayo inasisitiza kuwa mamlaka yote ya nchi itatokana na wananchi na kuwa wananchi ndiyo msingi wa mamlaka hiyo. Kwa kuwajengea uwezo viongozi wa mitaa, serikali inaongeza ushirikishwaji wa wananchi katika kutatua changamoto kwa njia za maelewano na si mabavu. Aidha, Ibara ya 107A(2)(e) ya Katiba inaeleza kuwa moja ya misingi ya haki ni kuhimiza matumizi ya mbinu mbadala za kumaliza migogoro. Hii ndiyo msingi wa “Utatuzi wa Mi...