Posts

Showing posts from May, 2025
Image
 SERIKALI YAWANOA MABALOZI NA WAJUMBE 8000 SONGEA: MIKAKATI YA KIKATIBA YA KUIMARISHA UTATUZI WA MIGOGORO KWA AMANI,DEMOKRASIA NA MASWALA YA UCHAGUZI MKUU UJAO Mpango wa kutoa elimu ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala kwa mabalozi na wajumbe wa serikali za mitaa unalenga kuimarisha misingi ya utawala bora, haki za binadamu, na amani ya kijamii kama inavyobainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (kama ilivyorekebishwa). 1. Msingi wa Kikatiba wa Mpango huu Mpango huu unajikita katika matakwa ya Ibara ya 8(1)(a)(b) ya Katiba, ambayo inasisitiza kuwa mamlaka yote ya nchi itatokana na wananchi na kuwa wananchi ndiyo msingi wa mamlaka hiyo. Kwa kuwajengea uwezo viongozi wa mitaa, serikali inaongeza ushirikishwaji wa wananchi katika kutatua changamoto kwa njia za maelewano na si mabavu. Aidha, Ibara ya 107A(2)(e) ya Katiba inaeleza kuwa moja ya misingi ya haki ni kuhimiza matumizi ya mbinu mbadala za kumaliza migogoro. Hii ndiyo msingi wa “Utatuzi wa Mi...

VIONGOZI SONGEA NA MADABA KUPATIWA ELIMU YA UTATUZI WA MIGOGORO SEKTA YA SHERIA

Image
  Wizara ya Katiba na Sheria imeandaa semina itakayotoa Elimu ya utatuzi wa Migogoro ya sekta ya Sheria kwa viongozi wa kada ya chini wa Manispaa ya Songea Mjini na wa Wilaya ya Madaba.   Akizungumza na Timu ya utoaji wa Elimu hiyo Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa ili kumaliza migogoro mbalimbali ya kisheria inayoibuka na ile iliyoibuliwa na Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ni vyema kuwapatia elimu viongozi hao ili wakabiliane nayo kuanzia ngazi za chini.   Aidha Mhe. Dkt Ndumbaro amesema mbali ya utatuzi wa Migogoro pia viongozi hao wapatiwe elimu ya uraia na Utawala bora, Elimu ya Ukatili wa Kijinsia na Elimu kuhusu Uchaguzi Mkuu.