Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria uliofanyika mjini Njombe ulihudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Pindi Chana, Naibu Waziri Jumanne Abdallah Sagini, na Katibu Mkuu wa Wizara, Bi. Marry Makondo. Wakiwa kwenye mazungumzo, viongozi hawa walijadili jinsi wananchi wanavyoweza kufaidika na kampeni hii ya msaada wa kisheria iliyoanzishwa na Mama Samia. Kampeni hii inalenga kutoa huduma za kisheria kwa wananchi, kuboresha upatikanaji wa haki na kuelimisha jamii kuhusu masuala ya kisheria.
VIONGOZI SONGEA NA MADABA KUPATIWA ELIMU YA UTATUZI WA MIGOGORO SEKTA YA SHERIA
Wizara ya Katiba na Sheria imeandaa semina itakayotoa Elimu ya utatuzi wa Migogoro ya sekta ya Sheria kwa viongozi wa kada ya chini wa Manispaa ya Songea Mjini na wa Wilaya ya Madaba. Akizungumza na Timu ya utoaji wa Elimu hiyo Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa ili kumaliza migogoro mbalimbali ya kisheria inayoibuka na ile iliyoibuliwa na Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ni vyema kuwapatia elimu viongozi hao ili wakabiliane nayo kuanzia ngazi za chini. Aidha Mhe. Dkt Ndumbaro amesema mbali ya utatuzi wa Migogoro pia viongozi hao wapatiwe elimu ya uraia na Utawala bora, Elimu ya Ukatili wa Kijinsia na Elimu kuhusu Uchaguzi Mkuu.

Comments
Post a Comment