Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria uliofanyika mjini Njombe ulihudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Pindi Chana, Naibu Waziri Jumanne Abdallah Sagini, na Katibu Mkuu wa Wizara, Bi. Marry Makondo. Wakiwa kwenye mazungumzo, viongozi hawa walijadili jinsi wananchi wanavyoweza kufaidika na kampeni hii ya msaada wa kisheria iliyoanzishwa na Mama Samia. Kampeni hii inalenga kutoa huduma za kisheria kwa wananchi, kuboresha upatikanaji wa haki na kuelimisha jamii kuhusu masuala ya kisheria.
WAKAZI WA ARUSHA WAJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA
Wakazi wa Mkoa wa Arusha wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika kampeni ya msaada wa kisheria iliyoanzishwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kampeni ambayo ilizinduliwa rasmi leo mkoani humo. Kampeni hii inalenga kuwawezesha wananchi kwa kuwapa elimu kuhusu haki zao za kisheria na kusaidia kutatua migogoro mbalimbali inayowakabili. Katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Paul Christian Makonda, waliongoza shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi. Kliniki za kisheria ziliwekwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa, ambapo wananchi walihudhuria kwa wingi na kupata fursa ya kushauriana na wataalamu wa sheria kuhusu changamoto zao, zikiwemo migogoro ya ardhi, mirathi, masuala ya kifamilia, na haki za kijinsia. Akizungumza na wananchi, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, aliwahimiza wakazi wa Arusha kutumia fursa hii muhimu...

Comments
Post a Comment