Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria uliofanyika mjini Njombe ulihudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Pindi Chana, Naibu Waziri Jumanne Abdallah Sagini, na Katibu Mkuu wa Wizara, Bi. Marry Makondo. Wakiwa kwenye mazungumzo, viongozi hawa walijadili jinsi wananchi wanavyoweza kufaidika na kampeni hii ya msaada wa kisheria iliyoanzishwa na Mama Samia. Kampeni hii inalenga kutoa huduma za kisheria kwa wananchi, kuboresha upatikanaji wa haki na kuelimisha jamii kuhusu masuala ya kisheria.



Comments

Popular posts from this blog

MSLAC YAZIDI KUIMARISHA UPATIKANAJI WA HAKI KWA WANANCHI NCHINI TANZANIA

VIONGOZI SONGEA NA MADABA KUPATIWA ELIMU YA UTATUZI WA MIGOGORO SEKTA YA SHERIA