Posts

Showing posts from March, 2025

MAELFU YA WATANZANIA SASA WANAELEWA HAKI ZAO NA WANAPATA MSAADA WA KISHERIA BILA GHARAMA.

Image
Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC) imeleta mageuzi makubwa katika utoaji wa elimu na msaada wa kisheria kwa wananchi wa Tanzania.   Kupitia kampeni hii, maelfu ya wananchi wamepatiwa elimu ya kisheria kuhusu haki zao za msingi, ikiwa ni pamoja na sheria za ardhi, mirathi, ndoa, ajira, na masuala ya kijinsia.   Mafunzo haya yamewasaidia wananchi kuelewa jinsi ya kulinda haki zao na wapi waende kupata msaada wa kisheria.  Upatikanaji wa Msaada wa Kisheria Bila Malipo   Kampeni hii imepeleka mawakili na wasaidizi wa kisheria kwenye mikoa mbalimbali ili kutoa msaada wa kisheria bila gharama kwa wananchi, hasa wale wa vijijini.   Wananchi wengi waliokuwa wakikosa haki zao kwa sababu ya ukosefu wa fedha sasa wanapata msaada wa kisheria bila gharama.     Kutatua Migogoro ya Ardhi na Mirathi  Kampeni hii imewezesha wananchi wengi kupata haki zao kwenye migogoro ya ardhi na mirathi kwa kutumia wanasheria na wasuluhishi ...

KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA - KIBAHA YATOA ELIMU KUHUSU HAKI NA USAWA KWA MAENDELEO YA TAIFA

Image
 

DAWATI LA MSAADA WA SHERIA LAREKEBISHA MIPAKA KATIKA ENEO LA UCHIMBAJI MAWE MLANGARINI

Image
Mlangarini, Arusha – Katika jitihada za kuondoa sintofahamu kuhusu mipaka ya eneo la uchimbaji mawe, Dawati la Msaada wa Sheria kwa kushirikiana na maafisa ardhi pamoja na afisa kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wamefika katika Kata ya Mlangarini kutoa elimu ya sheria na kusimamia upimaji upya wa eneo hilo.  Hatua hii imechukuliwa kufuatia mgogoro wa mipaka kati ya wanakijiji wa Mlangarini na Rikitesh Patel, mmiliki wa kiwanda cha kuchakata mawe kwa ajili ya kokoto. Patel alinunua eneo hilo kutoka kwa baadhi ya wenyeji wa kijiji, lakini kulizuka sintofahamu kuhusu mipaka halisi ya ardhi hiyo.   Wakati wa zoezi hilo, wataalamu wa ardhi walihakiki na kurejelea vipimo upya ili kuhakikisha haki inatendeka kwa pande zote na kuondoa migogoro isiyo ya lazima. Wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali na kupewa ufafanuzi wa kisheria kuhusu umiliki wa ardhi na taratibu sahihi za mauziano ya ardhi ili kuepuka changamoto za baadaye. Hatua hii imepokelewa vy...

WAZIRI NDUMBARO AONGOZA KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID ARUSHA, WANANCHI WANUFAIKA NA MSAADA WA KISHERIA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Dkt. Damas Ndumbaro, ameendelea kutoa huduma za msaada wa kisheria mkoani Arusha kupitia Kampeni ya Mama Samia Legal Aid. Huduma hizi zinatolewa katika viwanja vya TBA, zikiambatana na maadhimisho ya Wiki ya Wanawake Duniani yatakayofanyika Machi 8, 2025.   Katika kampeni hii, wananchi wamejitokeza kwa wingi kupata msaada wa kisheria. Miongoni mwao ni John Kaaya, mkazi wa Arusha, aliyefika Machi 2, 2025, katika mabanda ya Wizara ya Katiba na Sheria yaliyopo viwanja vya TBA, Arusha, ambapo alipatiwa msaada wa kisheria.  Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, amewataka wananchi kutoa maelezo sahihi kwa watoa huduma za msaada wa kisheria ili kufanikisha utatuzi wa changamoto zinazowakabili, hususan migogoro ya ardhi, mirathi, ndoa na masuala mengine ya kisheria. Aliyasema haya alipotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria mkoani Arusha kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.    Mkuu wa Mkoa wa Ar...

HAKUNA MWANANCHI ANAYEPASWA KUSALIA NA TATIZO LA KISHERIA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda, amewataka wananchi wa mkoa huo kuhakikisha wanatumia kikamilifu fursa ya msaada wa kisheria unaotolewa kupitia kampeni ya Mama Samia Legal Aid Campaign (MSLAC). Akizungumza Machi 3, 2025, Makonda ameonya kuwa hakuna sababu ya mwananchi kubaki na changamoto za kisheria bila kuzitatua, kwani mawakili na wataalamu wa sheria wanapatikana bure kupitia kampeni hiyo.  

WAKAZI WA ARUSHA WAJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA

Image
Wakazi wa Mkoa wa Arusha wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika kampeni ya msaada wa kisheria iliyoanzishwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kampeni ambayo ilizinduliwa rasmi leo mkoani humo. Kampeni hii inalenga kuwawezesha wananchi kwa kuwapa elimu kuhusu haki zao za kisheria na kusaidia kutatua migogoro mbalimbali inayowakabili.     Katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Paul Christian Makonda, waliongoza shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi. Kliniki za kisheria ziliwekwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa, ambapo wananchi walihudhuria kwa wingi na kupata fursa ya kushauriana na wataalamu wa sheria kuhusu changamoto zao, zikiwemo migogoro ya ardhi, mirathi, masuala ya kifamilia, na haki za kijinsia.   Akizungumza na wananchi, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, aliwahimiza wakazi wa Arusha kutumia fursa hii muhimu...