WAKAZI WA ARUSHA WAJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA
Wakazi wa Mkoa wa Arusha wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika kampeni ya msaada wa kisheria iliyoanzishwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kampeni ambayo ilizinduliwa rasmi leo mkoani humo. Kampeni hii inalenga kuwawezesha wananchi kwa kuwapa elimu kuhusu haki zao za kisheria na kusaidia kutatua migogoro mbalimbali inayowakabili. Katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Paul Christian Makonda, waliongoza shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi. Kliniki za kisheria ziliwekwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa, ambapo wananchi walihudhuria kwa wingi na kupata fursa ya kushauriana na wataalamu wa sheria kuhusu changamoto zao, zikiwemo migogoro ya ardhi, mirathi, masuala ya kifamilia, na haki za kijinsia. Akizungumza na wananchi, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, aliwahimiza wakazi wa Arusha kutumia fursa hii muhimu...







Tunampongeza na kumshukuru Rais wetu wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwa na muongozo mzuri katika kipindi hiki Cha uchanguzi ambapo kila mwananchi ana Haki ya kulindwa wakati wa uchaguzi,haki ya kushiriki kampeni za uchaguzi,haki ya kutoa malalamiko,haki ya kupiga kura na haki ya kugombea uongozi.
ReplyDeleteKampeni hii imesaidia sana kupunguza migogoro isiyo ya lazima
ReplyDeleteKila Mwananchi Anahaki ya kuchagua kiongozi anaye mtaka Hivyo kila Mtanzania Ana Haki ya kulindwa pindi anapo fanya Uchaguzi wa Kiongozi amtakaye anaye ona anamfaa
ReplyDelete